Open top menu
Friday, 27 May 2016


Mchezo huu uliopigwa kwenye dimba la taifa jijini Dar es salaam, ulishudia kikosi cha Yanga, ilipata ushindi wake kupitia kwa magoli ya mshambuliaji Amisi Tambwe aliyefunga bao la kwanza katika dakika ya tisa ya kipindi cha kwanza kisha akaongeza bao la pili katika dakika ya 47 ya kipindi cha pili .

Katika dakika ya 81 winga Deus Kaseke, alihitimisha kazi kwa kufunga bao la tatu baada ya kuunganisha krosi ya Simon Msuva.Bao la kufutia machozi la Azam,liliwekwa kambani na mshambuliaji Didier Kavumbagu.

Licha ya Yanga kushinda mchezo huu wa fainali Azam ndio wataiwakilisha Tanzania katika michuano ijayo ya kombe la shirikisho huku Yanga wakiwakilisha katika michuano ya klabu bingwa Africa.
Tagged
Different Themes
Written by Lovely

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments

Followers