Open top menu
Thursday 9 June 2016
Ni bajeti ya "HAPA KODI TUU"

Ikiwa ni bajeti ya kwanza ya serikali ya awamu ya tano iliyo chini ya utawala wa rais John Joseph Pombe Magufuli wasomi na wataalamu mbalimbali wa masala ya uchumi nchini wameonekana kuikosoa bajeti hiyo
bajeti hiyo iliyowasilishwa Juni 8 na Waziri wa Fedha Nchini Dkt. Philip Mpango imeonekana kuwakandamizi kwa masikini kinyume na vile ambavyo serikali ya awamu ya Tano imekuwa ikijinasibu
Abdul Shabani ni mtaalamu wa maswala ya uchumi ambapo yeye kwa upande wake anaimulika Bajeti hii kama ni kumnyonga mlala hoi "huwezi weka tozo ya asilimia 10 kwa miamala ya pesa kwa njia ya simu, huo ni unyonyaji" alinukuliwa Abdul
Pia alisisitiza kinyume na Matarajio ya wengi bajeti hiyo imejikita katika kuikusanyia Fedha serikali na wala sio kuwasaidia wananchi wa kipato cha chini hivyo basi kuwataka wabunge kutokuipitisha bajeti hiyo
kwa upande wake Jacob Alfred ambaye yeye Mfanyabiashara wa Gesi ameeleza kusikitishwa kwake na Bajeti hiyo kutokana na kile alichokieleza kuwa bajeti hiyo ina lengo la kuwafanya Watanzania kurudi kutumia Mkaa kwa wingi
"Wanatudanganya kuwa wanataka kuimarisha matumizi ya nishati mbadala, na kumfanya kila mtanzania aweze kutumia Gesi kama nishati mbadala lakini leo wamepandisha kodi katika gesi asilia, nimesikiliza majirani zetu Kenya wao wameshusha kodi kwa gesi asilia" alikaririwa Jacob
Bajeti ya Mwaka wa fedha 2016/2017 inakadiriwa kuwa shilingi Trilioni 29.5 huku kipaumbele kikubwa katika bajeti hiyo ikiwa ni ukusanyaji wa mapato kutoka kwa wananchi
Read more
Tuesday 7 June 2016
no image

CHUO CHA MUSOMA UTALII KINAKUTANGAZIA NAFASI ZA MASOMO
Read more
no image

Mimi ni moja wa wanachuo katika chuo hiki cha Musoma utalii Tawi la Tabora,vilevile ni msomaji na mfuatiliaji mzuri sana wa gazeti lenu napenda sana jinsi mnavyotuelimisha,kutuburudisha na kufichua maovu katika chuo na jamii nzima kwa ujumla.Habari zenu zinanivutia sana kwani napenda kufahamu mambo mbalimbali yanayojitokeza katika chuo na jamii vipengele vinavyonivutia ni Makala na Kurunzi la Mwandishi.
Ninapendezwa sana na Ujasiri mnaouonesha  wa Uandishi katika Habari Zenu,mnaonesha jinsi  mnavyowajibika nakuonesha umahiri wenu katika chuo hiki na si mimi tu! Mnawavutia wengi na baadhi yao wanatamani hata kubadirisha kozi mmekuwa mfano wa kuingwa.Naomba muendelee na uwajibikaji wenu mtafanikiwa sana na mtaweza kushindana katika soko la Ajira Natumaini mtakuwa waandishi wazuri wa habari ambazo zitakazowatetea wanyonge.
Kikubwa ninachopenda kuwashauri katika  Gazeti  lenu la Umoja ni mjitahidi kuboresha Habari Zenu ziwe na ukweli katika Uwandishi na msipende kuegemea upande mmoja ambapo itapelekea habari zenu kuwa na Usawa Mzidishe ubunifu zaidi na zaidi.Pia mjitahidi kulipanua Gazeti lenu lisiwe tu na wasomaji katika chuo chetu pekee.Liweze kusambaa na Mikoa mingine hii itapelekea waandishi wenu kujulikana kwa waandishi wa kimataifa.

Mungu awabariki muendelee kuwajibika zaidi katika fani yenu najua mnakutana na changamoto nyingi katika Harakati za kutupatia habari ambazo zitatujenga msichoke kupambana kwani tunawategemea sana.
Read more
Friday 27 May 2016
Yanga mabingwa wa shirikisho


Mchezo huu uliopigwa kwenye dimba la taifa jijini Dar es salaam, ulishudia kikosi cha Yanga, ilipata ushindi wake kupitia kwa magoli ya mshambuliaji Amisi Tambwe aliyefunga bao la kwanza katika dakika ya tisa ya kipindi cha kwanza kisha akaongeza bao la pili katika dakika ya 47 ya kipindi cha pili .

Katika dakika ya 81 winga Deus Kaseke, alihitimisha kazi kwa kufunga bao la tatu baada ya kuunganisha krosi ya Simon Msuva.Bao la kufutia machozi la Azam,liliwekwa kambani na mshambuliaji Didier Kavumbagu.

Licha ya Yanga kushinda mchezo huu wa fainali Azam ndio wataiwakilisha Tanzania katika michuano ijayo ya kombe la shirikisho huku Yanga wakiwakilisha katika michuano ya klabu bingwa Africa.
Read more
Tanzania ina upungufu wa sukari sasa hivi, imebidi Waziri mkuu aongee Bungeni


April 27 2016 Bunge limepitisha bajeti ya Makadilio ya mapato na matumizi ya fedha za ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka 2016/2017
Katika hotuba ya kuhitimisha bajeti hiyo, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alitoa hotuba na moja ya jambo lililowekewa msisitizo ni hii ishu ya kupanda bei kwa bidhaa ya sukari, Waziri Majaliwa hajalikalia kimya na kusema>>’

Ni kweli kwamba uzalishaji wa sukari nchini upo chini ya kiwango cha mahitaji, mahitaji ya sukari ni tani laki 4 na 20 na kiwango cha uzalishaji ni tani laki 3 na 20 hivyo tunaupungufu wa tani laki moja‘ –Waziri Mkuu Majaliwa

Sukari iliyokuwepo kwenye maghala yetu imepungua, lakini tumeshaagiza na ni ile tu ambayo imepungua, hivyo wananchi watambue sukari itaingia muda si mrefu kwa ajili ya mahitaji ya kitaifa‘ – Waziri Mkuu Majaliwa

Natoa maagizo kwa maafisa biashara wote wafanye ufuatiliaji kwenye maduka kuona kuwa sukari haifichwi na kuuzwa kwa bei ya juu, ni matumaini yangu kuwa Watanzania watanunua sukari ileile kwa bei elekezi‘ –Waziri Mkuu Majaliwa

ULIIKOSA RIPOTI YA TUHUMA ZA RUSHWA TANZANIA NA MENGINE YA WAZIRI MKUU AKIWASILISHA BAJETI? TAZAMA HII VIDEO HAPA CHINI..
Read more
Rais Magufuli kujaza vijana Serikalini, amegudua haya kwa vijana..

Kila siku asubuhi huwa nazisogeza headlines zilizobebwa kwenye kurasa za Magazeti ya Tanzania, Uchambuzi wa stori zote napandisha kwenye account yangu ya Twitter>>>@millardayo na Zote nakusogezea hapa chini.

Moja ya stori kubwa ni hii ya gazeti la Nipashe yenye kichwa cha habari ‘Magufuli kujaza vijana Serikalini‘ Gazeti hili limeripoti kuwa Magufuli amesema kuanzia sasa wateule wengi wa Serikali watakuwa vijana kwa kuwa amegundua wengi hawapendi rushwa.

Gazeti hilo limeongeza kauli ya Rais Magufuli kuwa anafahamu kwamba vijana hawapendwi lakini amegundua ndio wachapakazi ambao watasaidia kulipeleka Taifa katika maendeleo anayoyatamani kwani aliowaweka tayari ameshaanza kuona matunda ya kazi zao.

Rais Magufuli aliyasema hayo wakati wa ufunguzi wa mkutano wa makandarasi wa mikoa ya Dar es salaa, Mbeya na Dodoma.
Read more
JOSE MOURINHO ASAINI KUIFUNDISHA MAN UNITED


Uongozi wa Man United leo May 27 2016 umetangaza rasmi kumpa mkataba wa miaka mitatu, kocha wa zamani wa klabu ya Chelsea Jose Mourinho wenye kipengele cha kubaki katika klabu hiyo hadi mwaka 2020.
Jose Mourinho ametangazwa na klabu hiyo lakini atajiunga na kuanza kufanya kazi rasmi msimu wa mwaka 2016/2017 hii ina maana tutaanza kumuona Mourinho akiiongoza Man United  kama kocha mkuu wakati wa mechi za maandalizi ya mechi za msimu.
Kama utakuwa unakumbuka vizuri Jose Mourinho alifukuzwa kazi na Chelsea December 2015,  kocha huyo mwenye asili ya Ureno toka mwaka 2003 hadi sasa akiwa kama kocha amefanikiwa kushinda jumla ya Makombe 23 katika nchi 4 tofauti.
Read more
Tuesday 24 May 2016
Diamond kwenye headlines nyingine na Wizkid, AKA, Drake, Beyonce na Rihanna

May 20 2016 Tanzania imeamka na habari nyingine njema za Diamond Platnumz kuchaguliwa tena kushiriki kwenye tuzo za kituo maarufu cha TV Marekani kiitwacho BET ambapo Platnumz amekua na mwaka mwingine mfululizo wa kuwa nominated na sasa ni kwenye tuzo za BET Awards 2016.

Diamond ameshukuru kwa kuchaguliwa kuwania tuzo kwenye kipengele cha Best international Act Africa ambapo ameyaandika maneno haya baada ya kufikiwa na taarifa >>> ‘Ningependa niwashukuru kwa Sapoti kubwa Manayozidi kunipa na niwajuze kuwa kijana wenu nimechaguli kuwania tunzo ya Msanii Bora wa Kimataifa toka Africa kwenye tunzo za BET #BETAwards America’

Tuzo za BET 2016 ambazo zitatolewa nchini Marekani zimeanza kuchukua nafasi kwenye headlines baada ya kutangazwa list ya waliochaguliwa kuwania huku Beyonce, Rihanna na Drake wakitangazwa kuongoza kwa kuwania tuzo zaidi ya moja.
Read more
Makundi ya Klabu Bingwa na Kombe la Shirikisho Afrika yamepangwa, Yanga yupo Kundi A

Baada ya kumalizika kwa hatua ya mtoano ya michezo ya Kombe la Shirikisho na Klabu Bingwa barani Afrika, leo May 24 2016 shirikisho la soka barani Afrika CAF na ilichezesha droo ya kuzipanga timu hizo zilizosalia katika Makundi mawili ya A na B.

Kwa upande wa Tanzania Yanga ndio inawakilisha Taifa, nafasi ambayo iliipata baada ya kuitoa GD Esperanca ya Angola kwa jumla ya goli 2-1 katika hatua ya 16 bora.
Read more

Followers