Open top menu
Tuesday 7 June 2016

Mimi ni moja wa wanachuo katika chuo hiki cha Musoma utalii Tawi la Tabora,vilevile ni msomaji na mfuatiliaji mzuri sana wa gazeti lenu napenda sana jinsi mnavyotuelimisha,kutuburudisha na kufichua maovu katika chuo na jamii nzima kwa ujumla.Habari zenu zinanivutia sana kwani napenda kufahamu mambo mbalimbali yanayojitokeza katika chuo na jamii vipengele vinavyonivutia ni Makala na Kurunzi la Mwandishi.
Ninapendezwa sana na Ujasiri mnaouonesha  wa Uandishi katika Habari Zenu,mnaonesha jinsi  mnavyowajibika nakuonesha umahiri wenu katika chuo hiki na si mimi tu! Mnawavutia wengi na baadhi yao wanatamani hata kubadirisha kozi mmekuwa mfano wa kuingwa.Naomba muendelee na uwajibikaji wenu mtafanikiwa sana na mtaweza kushindana katika soko la Ajira Natumaini mtakuwa waandishi wazuri wa habari ambazo zitakazowatetea wanyonge.
Kikubwa ninachopenda kuwashauri katika  Gazeti  lenu la Umoja ni mjitahidi kuboresha Habari Zenu ziwe na ukweli katika Uwandishi na msipende kuegemea upande mmoja ambapo itapelekea habari zenu kuwa na Usawa Mzidishe ubunifu zaidi na zaidi.Pia mjitahidi kulipanua Gazeti lenu lisiwe tu na wasomaji katika chuo chetu pekee.Liweze kusambaa na Mikoa mingine hii itapelekea waandishi wenu kujulikana kwa waandishi wa kimataifa.

Mungu awabariki muendelee kuwajibika zaidi katika fani yenu najua mnakutana na changamoto nyingi katika Harakati za kutupatia habari ambazo zitatujenga msichoke kupambana kwani tunawategemea sana.
Tagged
Different Themes
Written by Lovely

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments

Followers