Open top menu
Thursday 19 January 2017

Mkuu Wa Chuo Cha MusomaUtalii Ally Nyambi
Maktaba kwa ajili ya kujisomea katika chuo cha Musoma Utalii (MUC) inatarajiwa kuanza kutumika rasmi kuanzia tarehe moja ya mwezi wa nane mwaka huu
Hayo yamebainishwa na mkuu wa chuo hicho Ally Nyambi siku ya Ijumaa katika mkutano maalumu kati ya wanachuo na uongozi wa chuo hicho (College baraza) wakati wa kujibu maswali yanayowatatiza na kuwahusu wanachuo hao
Akijibu swali la Mgecha Safari Mussa mwanafunzi wa elimu ya awali chuoni hapo aliyetaka kujua ni lini Maktaba iliyopo chuoni hapo itaanza kutumika, mkuu huyo wa chuo alieleza kuwa maktaba hiyo itaanza rasmi kutumika mnamo Agosti 1, 2016
“Ni kweli kabisa mmekuwa mkipata shida pale mnapotaka kujisomea, Uongozi wa chuo umeliona hilo na kulifanyia kazi, tunayo maktaba ya kisasa kabisa ambayo imekalika na tunasubiri Tarehe moja ya mwezi ujao ili ianze kutumika” alisema mkuu huyo wa chuo
Pia mkuu huyo wa chuo alisisitiza kuwa katika Maktaba hiyo kuna vitabu mbalimbali ambavyo vitakidhi mahitaji ya wanachuo hao na kuwataka wanachuo hao waanze kujijengea tabia ya kujisomea
Pamoja alibainisha kuwa uongozi wa chuo umeandaa kanuni mbalimbali za kufuatwa na wananchuo ili kuweza kuruhusiwa kutumia Maktaba hiyo huku akisisitiza kuwa hakuna mwanachuo atakaye ruhusiwa kuingia kujisomea katika maktaba hiyo bila ya kuwa na vitambulisho
“Pamoja na kuwa kutumia maktaba ni haki yenu, ila hakuna kitu kinachoenda bila ya kuwa na utaratibu, hivyo basi kuna kanuni na taratibu ambazo tumezipanga na mta bandikiwa kwenye ubao wa matangazo mzione, ila mojawapo ni kwamba hakuna mwanafunzi atakayeingia maktaba bila ya kuwa na kitambulisho” alikaririwa mkuu huyu wa chuo
Mkutano baina ya wanachuo katika chuo cha Musoma Utalii - Tabora na uongozi wa chuo hicho ulifanyika ijumaa ya Julai 16, 2016 katika ukumbi wa Nyerere chuoni hapo



Tagged
Different Themes
Written by Lovely

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments

Followers